Deutsche Post DHL Group

Utiifu wa kanuni ni jambo la lazima katika Deutsche Post DHL Group. Utiifu wa kanuni ni wajibu wa kila mtu!

Lengo letu la kipekee ni kufanya biashara halali na inayoyofuata maadaili bora! Sisi sote tuna jukumu la kudumisha lengo hili.
Ninakuhimiza uripoti shughuli yoyote isiyo halali au mwenendo mbaya unaotiliwa shaka. Unaweza kufanya hivyo kupitia mfumo huu wa BKMS® System na usaidie kampuni yetu.
Ukikishuhudia, kiseme, ili tuweze kukikomesha!

Kutii kanuni kunahusu hasa kufanya jambo sahihi na kunamaanisha kufuata sheria, kanuni na sera za ndani, kama vile Kanuni yetu ya Maadili, Kanuni ya Maadili ya Msambazaji wetu au Taarifa ya Sera ya Haki za Binadamu. Kutii kanuni katika Deutsche Post DHL Group ni muhimu katika kudumisha hali ya kuwa Mwajiri, Mtoa Huduma na Mwekezaji Bora.

Hatua ya kutotii mojawapo ya viwango vyetu vovyote inaweza kusababisha madhara makubwa kwetu sote!

Kwa hivyo, wakati wowote unapotilia shaka mwenendo wowote mbaya, tafadhali usichelewe kuripoti kwa kutumia mfumo huu wa BKMS® System System au njia nyingine zilizotolewa kwenye ukurasa huu! Njia hii pia inakupa uwezo wa kuripoti masuala bila kutambuliwa.

Tafadhali kumbuka kuwa mfumo huu haushughulikii malalamiko ya huduma yanayohusiana na usafirishaji wa bidhaa. Malalamiko kuhusu usafirishaji wa bidhaa yanapaswa kuwasilishwa kwa vituo husika vya mawasiliano vya Deutsche Post
(https://www.deutschepost.com/en/business-customers/contact.html)
au DHL
(https://www.dhl.com/global-en/home/contact-us.html).

Kwa nini ninapaswa kuwasilisha ripoti?
Ni aina gani ya ripoti zinazoweza kuwasilishwa kupitia mfumo huu?
Mchakato wa kuwasilisha ripoti ni upi? Kisanduku pokezi ni nini na ninawezaje kukisanidi?
Ninapaswa kutumia njia gani ili kuwasilisha ripoti?
Ni nani atakayepokea ripoti yangu? Nitahakikisha aje kuwa sitalipizwa kisasi?
Ninawezaje kupokea majibu na niendelee kutotambulika kwa wakati mmoja?
Mchakato wa kuwasilisha ripoti kwa njia ya simu hutumika vipi na mfumo wa BKMS® VoiceIntake?
Ninaweza kuripoti matukio ya ufichuzi haramu wa data kupitia njia hii?
Ninaweza kuripoti unyanyasaji kupitia njia hii?